KAMPUNI ya Kuhifadhi Mafuta nchini (TIPER) imekabidhi hundi ya Sh
bilioni 1 kwa Serikali, ikiwa ni sehemu ya gawio la Serikali katika
faida iliyotengenezwa hadi kufikia Desemba 31, mwaka jana. Kampuni hiyo
inamilikiwa kwa ubia baina ya Serikali na Kampuni ya Uswisi ya Oryx
(OOG), kila moja ikiwa na hisa 50, imekuwa ikilipa gawio kama hilo tangu
mwaka 2009 baada ya uwekezaji wa Sh bilioni 8.3 ambao uliwezesha
kufanya kazi kwa faida.
Kampuni hiyo ililipa gawio la Sh bilioni 1.3 mwaka 2009, bilioni moja katika mwaka 2010 na bilioni 2 katika mwaka 2011.
Akizunguzuma
wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi hiyo jijini Dar es Salaam
mwanzoni mwa wiki, Mkurugenzi Mtendaji wa TIPER, Daniel Belair, alisema
mchango wa gawio toka katika kampuni hiyo utakuwa chachu ya maendeleo ya
uchumi nchini.
“Tunayo furaha kukabidhi hundi hii yenye thamani
ya shilingi bilioni 1 ikiwa ni wajibu wetu kisheria kama kampuni.
Tunaamini mchango wetu utasaidia kuchochea mchakato wa maendeleo ya
uchumi wa taifa kwa ujumla,” alisema Belair.
Alisema TIPER
inatarajia kuongeza zaidi uwezo wake wa kuhifadhi mafuta ili kufikia
zaidi ya mita za ujazo 290,000 ifikapo mwaka 2015, baada ya uwekezaji wa
Dola za Marekani bilioni 12.
Belair alisema hadi sasa TIPER ina
kituo kikubwa cha kuhifadhi mafuta nchini chenye uwezo wa kuhifadhi mita
za ujazo zaidi ya 141,000, ikilenga kufikia mita za ujazo 215,000 kwa
siku za baadaye.
“Katika uwekezaji mpya, tenki mbili zenye uwezo
wa kuhifadhi mita za ujazo 36,600 zimeshaongezwa katika robo ya kwanza
ya 2013. Kipaumbele chetu kikubwa ni kuhakikisha kuwa bidhaa za mafuta
ya petroli zinapatikana katika soko muda wote,” alisema.
Alisema
katika mwaka wa fedha wa 2011/2012, kampuni yake ilijikita katika miradi
mbalimbali ya kusaidia jamii katika sekta za elimu na afya, ikiwa ni
sehemu ya sera ya kampuni yake ya kusaidia jamii inayoizunguka kampuni.
Akipokea
hundi hiyo kwa niaba ya Serikali, Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa,
aliitaka kampuni ya TIPER iendelee kufanya kazi kwa juhudi na
kuihakikishia bodi ya kampuni hiyo kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono
jitihada zake.
“Tuna furaha kwa kupata mchango huu wa gawio,
kwani ni wakati muafaka. Msisite kuifuata wizara yangu kwa jambo lolote
linalohitaji msaada wetu,” alisema
BONGO NEWS 4 NEWS#
No comments:
Post a Comment