Kikao cha kamati ya utendaji cha klabu hiyo kilichoketi jana kimeamua kupinga hatua hiyo ya Azam media kupewa haki hizo za televisheni na bodi ya ligi kuonesha ligi kuu kwa miaka mitatu kutokea msimu ujao utakaoanza kuunguruma August 24.
Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Mehboob Manji amesema mkataba huo hauko wazi wenye mgongano wa kimaslahi,kwakuwa kampuni hiyo ndio inayoimiliki Azam FC ambao ni maadui wakubwa wa Yanga uwanjani.
Manji amelalamikia pia bodi hiyo ya ligi ambayo iko kwa mpito kabla ya kufanyika kwa uchaguzi akisema haina mjumbe hata mmoja kutoka klabu ya Yanga.
BONGO NEWS 4 NEWS#
No comments:
Post a Comment