Pages

Monday

Baada Ya Kuwachana Watu Vilivyo Katika Ngoma Yake Mpya Ya Salam Zao, Haya Sasa Ndio 'Mabalaa' Yaliyoanza Kumpata Ney Wa Mitego


Tokea kutoka kwa Wimbo mpya wa Ney wa Mitego, Salam Zao Story ni kwamba msanii huyu sasa amejikuta akipokea vitisho mbalimbali hasa kupitia message za simu kutoka kwa watu wakiwepo wadau wakubwa wa game ya muziki hapa Bongo.



Msanii huyu amesema kuwa message hizi zimetoka kwa watu ambao wanafahamika, na pia zile ambazo zimemfikia bila kuwa na majina, anafurahi kwasababu kuna uwezekano wa kufuatilia na kuwatambua ni nani waliotuma ujumbe huo.
    
Ney amesema kuwa kwa sasa ana message kama nne tofauti za aina hii, ambazo yeye binafsi amesema hazimtishi chochote na anaona waliochukua hatua ya kumtumia , watakuwa wame-panick kutokana na ujumbe alioutoa kuwagusa moja kwa moja.
        

Msanii huyu amesema kuwa, Kitendo hiki cha kumtishia kupitia ujumbe wa simu ukiendelea atafanya maamuzi ya kuziweka wazi kwa watu, ambapo kuanzia leo ameanza kuweka wazi message moja moja mtandaoni.

Ney pia ameenda mbele zaidi na kuchana live kuwa watu wakwanza kuanza ku-panick kutokana na ujumbe mzito kutoka ngoma yake ni wahusika wa msiba wa Marehemu Mangwea na wale wa Marehemu Kanumba ambao katika message zao wametaja na mambo mengine maovu mengi panmoja na wahusika wake.

No comments:

Post a Comment