John Davison Rockefeller ndiyo mtu tajiri
sana katika historia ya dunia hadi leo, unaambiwa utajiri wake
ukifananisha na hawa matajiri wa karne hii amewaacha mbali kupita kiasi,
ukichukua utajiri wa Bill Gates na Carlos Slim ambao wote kwa pamoja
wana utajiri wa billioni 140 bado hawatafikia hata nusu ya utajiri
aliowahi kuwa nao huyu jamaa.
Mwaka 2007 mtandao wa Forbes ulirekebisha
utajiri wa John Rockefeller baada ya inflation (mfumuko wa bei) na
kukadiria kwamba alikuwa na utajiri wa dolla billion 663.4
John Rockefeller alifariki mwaka 1937 May
23 huko Florida akiwa na miaka 97, utajiri wake umetokana sana na
biashara ya mafuta ambayo kwa kipindi hicho ndiyo ilikuwa nishati mpya
na inahitajika sana, alianzisha kampuni inaitwa Standard Oil Company
ambayo iliweza kufanikiwa kutawala soko la mafuta kwa kiasi kikubwa
sana, baada ya biashara kwenda vizuri akiwa na ndugu zake wa karibu…
John Rockefeller aliweza kuwa Mmarekani wa kwanza kufikisha utajiri wa
dola billioni moja.
Zaidi ya biashara, John Rockerfeller
alitumia utajiri wake mwingi kwenye ku-invest ndani ya masuala ya
utafiti wa kisayansi kwenye mambo ya dawa za binadamu, elimu na kusaidia
watu kwenye foundation yake ambapo kwenye research alizowahi kuwekeza
pesa zake na kuweza kupata mafanikio makubwa hasa kwenye kutokomeza
janga la homa ya manjano kipindi hicho na minyoo inayoitwa hookworm.
Kumbukumbu ya John Rockefeller kwenye sekta
ya elimu bado ipo hadi leo kwasababu ndiye mwazilishi wa vyuo vikuu
vitatu huko Marekani ambavyo ni University of Chicago, Rockerfeller
University na Central Philippine University.
BONGO NEWS 4 NEWS#
No comments:
Post a Comment