Pages

Saturday

PHOTOS: Picha za “utata” za prodyuza Manaiki Sanga na wasanii wa kike zavuja


PRODYUZA mkali Bongo, Manaiki Sanga amekumbwa na skendo ya aibu kufuatia picha zake chafu akiwa na wasichana wanaodaiwa ni wasanii wa filamu kusambaa mitandaoni huku wachangiaji wakisema ni udhalilishaji uliopitiliza, Risasi Jumamosi limezinasa.


Picha hizo mbalimbali zinamuonesha Manaiki na wasanii hao wakiwa katika mapozi tofauti huku wakiashiria kwamba walikuwa wanajua wanarekodiwa.
Baadhi ya picha zinamuonesha prodyuza huyo akiwa na msanii mmoja, tangu ana nguo zake zote kisha kuanza kuzivua moja baada ya nyingine hadi kubaki kama alivyozaliwa.
Matukio hayo yote yalifanyika ndani ya chumba kimoja ambacho haijajulikana kama ni hotelini, gesti au nyumbani kwa prodyuza huyo lakini hisia za macho zinasema ni sehemu ngeni na makazi yake.
Kumbukumbu za nyuma zinaibua mahojiano kati ya prodyuza huyo na mtangazaji wa redio moja ya jijini Dar, akiulizwa kuhusu taarifa kwamba amekuwa na tabia ya kupiga picha chafu ambapo majibu yake yalikuwa yakijigongagonga.
Ili kuupata ukweli wa picha hizo ambazo nyingi zinazua kichefuchefu kiasi cha kushindwa kutumika gazetini, juzi, Risasi Jumamosi lilimsaka Manaiki kwa njia ya simu ya mkononi ambapo alipopatikana na kusomewa mashitaka alisema:
“Mi sijui lolote bwana, wala sijaziona kwanza.”
Risasi: Yaani picha za kwako halafu unasema hujaziona, si ulipiga wewe?”
Manaiki: Kwani zimetapakaa kwenye mtandao gani?”
Alipotajiwa jina la mtandao mmoja tu kati ya mingi yenye picha hizo, prodyuza huyo alisema anamfahamu mmiliki wake hivyo atampigia simu muda si mrefu.
Baada ya nusu saa, Manaiki alipigiwa tena simu lengo likiwa kujua kama aliongea na mmiliki wa mtandao huo alisemaje, lakini simu iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa. 

CREDIT GLOBAL PUBLISHERS
BONGO NEWS 4 NEWS#

No comments:

Post a Comment