Pages

Monday

Diamond Platnumz - Number One (Official Video Music) HII HAPAAA....!!!



Video ilio kua iki subiriwa kwa hamu hapa bongo kutoka kwa mtoto wa Kigoma (Diamond plutnumz) ndio hiyo hapo chukua wakati wako ama nafasi yako kuweza kuicheki ilivyo tulia.
BONGO NEWS 4 NEWS#

Sunday

SERENGETI FIESTA 2013 MKOANI MTWARA NOOOOOMAAAA SAAAANAAAAA



Wakazi wa Mtwara wajitokeza kwa wingi katika Tamasha la Burudani la Serengeti Fiesta 2013.
Dj Mully B akiporomosha mawe katika tamasha la serengeti Fiesta 2013 Mtwara.
Haya sasa naona viduku vimetawala hapa kwa wakazi wa Mtwara

OZIL MBIONI KUJIUNGA NA ARSENAL KWA ADA YA UHAMISHO WA £42M KUTOKA REAL MADRID


Klabu ya Arsenal io mbioni kukamisha usajili wa kiungo wa Real Madrid Mesut Ozil katika siku ya mwisho ya usajili barani ulaya.
Kwa mujibu wa ripoti zilizoenea mitandaoni ni kwamba Arsenal wapo katika mazungumzo ya mwisho na Real Madrid juu ya usajili wa Ozil .

Kiungo huyo wa kijerumani mwenye miaka 24 amekuwa Bernabeu tangu mwaka 2010 akitokea Werder Bremen.
Na Ozil anaweza kuelekea Emirates Stadium baada ya Gareth Bale kujiunga rasmi na miamba ya soka la Hispania akitokea Tottenham kwa ada ya uhamisho iliyovunja rekodi ya £85.3m.
Ozil ameshaitumikia Madrid katika michezo zaidi ya 100 huku akiwa na rekodi ya kuongoza kwa assists nyingi zaidi barani ulaya katika misimu mitatu iliyopita.

BAADA YA MIAKA 37 (2050) DUNIA YETU ITAKUWA HIVI....



Hili ni Swali ambalo kila Mtu anapaswa kujiuliza Moyoni Mwake! Ukweli ni kwamba kwa wenzetu si kama tunavyofikiri, wameshatengeneza au kubuni dunia ya mwaka 2050 itakavyo kuwa, na itakuwa ni Dunia ya ajabu iliyojawa na maajabu ya wanadamu  watakao kuwepo wakati huo. Utafiti wetu unaonyesha kwamba Kampuni Ya MICROSOFT imeshandaa mpango huo na wameupa jina la  Microsoft 2050 target technology.


MICROSOFT 2050 TARGET TECHNOLOGY
BONGO NEWS 4 NEWS#

KILI MUSIC TOUR 2013 YAVUNJA REKODI YA MAHUDHURIO KATIKA UWANJA WA LAKE TANGANYIKA MKOANI KIGOMA! CHEKI PICHA 30 HIZI HAPA


Ziara ya wanamuziki waliofanya vizuri mwaka 2012 maarufu kama Kilimanjaro Music Tour 2013 iliyopewa kaulimbiu ya Kikwetu kwetu imefanyika mkoani Kigoma na kuvunja rekodi ya mahudhurio katika uwanja wa Lake Tanganyika baada ya maelfu ya
wakazi wa mji wa Kigoma na maeneo ya jirani kufurika kwa wingi kuwashuhudia wasanii wakali 12 waliopanda jukwaani. Kivutio kikubwa katika tamasha hilo ilikuwa ni wanamuziki wanne wanaounda kundi la Kigoma All Stars, Diamond, Mwasiti, Linex na Recho kupanda mwishoni na kuimba wimbo wao maarufu wa Leka Dutigite na kupata shangwe kubwa toka kwa mashabiki. Hizi ni baadhi ya picha za matukio yaliyotokea.


 Diamond Platnumz akifanya kufuru jukwaani... Hapo ametengeneza umbo la ndege...


 Profesa Jay wa mitulinga..
 Yahaya unaishi wapi?... yahayaeeeeee..... Lady Jay Dee akikamua.
 DJ Akishusha mkong'oto!
 Linex akiwanyanyua mashabiki kwa mistari yake yenye hisia kali...
 Roma mkatoliki kushoto, Mkurugenzi wa Kili music tour katikati na Mwasiti kulia wakionyesha batasam! A! tabasam la nguvu...
 Fid Q Akiporomosha mistari ya kufa mtu..
 Warembo pia walikwepo...
 DJ Wa kilimanjaro music tour akiwarusha watu wa kigoma.
 Mashabiki wakionyesha ishara ya kumpokea Izzo vizuri...
 Izzo Akifanya yake
 Ben Paul Jukwani
 Izzo busnnes akiwa backsage na kinywaji vuguvugu..
 Mwasiti huyo
 Mwasiti akifanya makeke jukwaani..
 Barnaba boy akikamua..
 Recho akifanya yake