Pages

Friday

PAPA FRANCIS ATOA SALAMUZA EID KWA WAISLAMU WOTE DUNIANI


Papa Francis 
apa Francis, amewatakia Waislamu wote duniani, sikukuu njema ya Eid el- Fitr huku akiwahimiza kuheshimiana zaidi kupitia elimu.
“Mwaka huu wa kwanza kama kiongozi wa Kanisa Katoliki, nimeamua kutuma ujumbe huu kwenu marafiki zangu Waislamu nikiwa na heshima kubwa. Ninatambua uhusiano, udugu na urafiki baina yetu sisi,” alisema Papa Francis katika salamu zake.
Makao ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani, yameulezea waraka huo kuwa ni wa salamu maalumu za Sikukuu ya Eid al-Fitr inayofanyika duniani leo, baada ya kumalizika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

LADY JAYDEE ARUSHA TOUR: PICHA ZAKE ZA KWANZA AKIWA HUKO A.TOWN HIZI HAPA...


Siku ya leo mkoani Arusha kutakua na bonge la show litakalo dondoshwa na msanii Lady jdee (Anaconda) ndani ya ukumbi wa triple Akingilio kikiwa n sh.10,000 tu.Kwa wale wa karibu na hata mbali itawahusu na ina wahusu kwa saa..na.Hizi ndizo picha baadhi alizo photoa akiwa maeeno hayo na wadau kadhaa hivi cheki mwenyewe.

MMILIKI WA LIVERPOOL ASEMA "KUWAUZIA SUAREZ ARSENAL UTAKUWA NI UPUMBAVU - HAENDI POPOTE DIRISHA HILI LA USAJILI."


Luis Suarez amezidi kupata vizingiti vikubwa katika harakati zake za kutaka kuhama Liverpool, baada ya kuambiwa na mmiliki wa Liverpool John Henry warning: “Huendi popote”.

VIGOGO WAWILI WA BANWA KU KAMATWA KWA AGNES MASOGANGE NA MADAWA...


HABARI zilizochimbuliwa kwa undani zinadai kuwa tayari vigogo wawili waishio nchini wamebanwa na Jeshi la Polisi Tanzania wakituhumiwa kumtuma Masogange kupeleka madawa ya kulevya nchini Afrika Kusini.

Thursday

DIVA WA CLOUDS FM AFUNGUKA TENA ASEMA HAJAWAHI ONA MWANAUME KAMA PREZOO



Kwa  mara  nyingine  tena,  mtangazaji  wa  Clouds fm  maarufu wa  jina  la  DIVA  amejitosa Istagram  na  kuanza  kuisifia  suruali yake ( Prezzo)  huku  akiwaponda  wanaume  wa  kibongo  na  wale  wote  wanaomchukia  Prezzo....

Huu  ni  ujumbe wake.

PICHA ZA UTENGENEZAJI WA VIDEO MPYA YA DIAMOND SOUTH AFRICA.


EXCLUSIVE : PICHA ZA VIDEO MPYA YA DIAMOND ANAYOIFANYA SOUTH AFRICA

RAY C ASIMULIA KILICHOMFANYA AANZE KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA........LAWAMA ZOTE AMEZIELEKEZA KWA MPENZI WAKE



 
 Muimbaji wa ‘Niwe Nawe Milele’ Rehema Chalamila aka Ray C jana alifanya interview ya kwanza ya TV tangu takriban miezi 10 iliyopita baada ya kujichimbia kupata matibabu ya madhara aliyokuwa amepata kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya.

IRENE PAUL ADAIWA KUWA MJAMZITO...

Staa wa filamu za Kibongo,Irene Paul amedaiwa kuwa mjamzito ambapo inasemekana amekuwa akiuficha ujauzito huo ili asipigwe picha na mapaparazi.

Zivunje laana za kurithi ktk ngono na mapenzi

harusi-ndoa-wapenzi-couple 
Leo nataka tuongelee laana za kurithi..wengi tukifikia hapa tunajisahau kabisa haswa kwenye mambo ya ndoa na uzazi, wakati unataka kuolewa je unakuwa umevunja laana za ulipotoka?? na ulipo je umevunja laana za wazazi na mababu ambazo zimekuwa kwenye damu yako??? unajikuta mtu umepata mume unaolewa halafu mama yako hajawahi kuolewa 

MUME WA PILI WA WASTARA AIBUKA


MIEZI nane baada ya kufariki dunia mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’, hatimaye mume wa pili wa staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma aitwaye Ahmed Kushi ameibuka na kudai kwamba anatambua kwamba staa huyo bado ni mkewe na anataka ampatie mwanaye aliyezaa naye.
Kwa muda mrefu kulikuwa na taarifa kuwa Wastara aliachana na mwanaume huyo kwa talaka kabla ya kuolewa na Sajuki lakini kuibuka kwake na madai kuwa bado mwanadada huyo ni mkewe kumezua mshangao mkubwa.

Huyu Ndiye Mwigizaji Wa Kike anae ongoza Kwa Kulipwa Pesa Nyingi, soma kujua ana lipwa shilingi ngapi Katika Filamu Moja



Mwigizaji mkongwe, Angelina Jolie ametajwa kama ndiye mwigizaji wa kike anayelipwa zaidi duniani licha ya mwanadada huyu kutokutokea katika filamu hususan katika nafasi ya uhusika mkuu toka mwaka 2010 katika filamu maarufu ya 'The Tourist'

MFANYA BIASHARA WA MADINI APIGWA RISASI MOSHI.



                                    Mwili kulia mara baada ya kupigwa risasi.

Wednesday

WANAMUZIKI 10 MATAJIRI AFRIKA

DbanjMUZIKI ni kazi, mataifa mengi, hususan katika mabara ya Ulaya na Amerika Kaskazini, umewatajirisha vijana wengi.

TAZAMA PICHA ZA TUKIO LA KUUNGUA KWA MOTO UWANJA WA NDEGE WA JOMO KENYATA


Moto mkubwa unaripotiwa kuzuka asubuhi hii katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyetta (JKIA) jijini Nairobi.

ALIYE FANYA MAPENZI NA NANDO ( SELY) AMUOMBA MSAMAHA MPENZI WAKE


Hatimaye mshiriki wa Ghana katika reality show ya Big Brother ‘The Chase’ Selorm Galley maarufu kama Selly aliyetoka wiki moja iliyopita, amemuomba msamaha boy friend wake (wa Ghana) kwa yale aliyoyafanya mbele ya Camera za nyumba ya Big Brother.

Tuesday

PICHA: DIAMOND AFANYA SHOOTING YA NYIMBO YAKE MPYA AKIWA NA MIONGONI YA GARI ZENYE GHARAMA KUBWA DUNIANI HUKO AFRIKA KUSINI

bef82682fdd111e2a8b522000a9f3cba_7

Bongo Flava Prince, Diamond Platnumz yupo nchini Afrika Kusini kishule na kikazi pia. Staa huyo wa Kesho ameshoot video ya wimbo wake mpya ambao bado haujulikani ni upi mpaka sasa.

PICHA: TAZAMA RIHANNA ALIVYOVAA MAVAZI YA AJABU AJABU KATIKA SHEREHE ZA CROP OVER CARNIVAL

4c5be146fde911e2816522000a9e48f9_7



Rihanna ameuangana na wananchi wengine wa nchi mwake Barbados kufurahia tamasha la kila mwaka la Crop Over Carnival. Akiwa amevalia mavazi kama wanawake wa Kizulu wa nchini Afrika Kusini, Riri alionekana mwenye furaha na kwenye picha moja wapo aliyopost kwenye Instagram, aliandika kuwa anaipenda nchi yake.

MSIMAMO WA RAIS KIKWETE KWA RAIS KAGAME WA RWANDA WAUNGWA MKONO KWA ASILIMIA 100 NA WASOMI HAPA NCHINI


 WASOMI  na  baadhi  ya  wanasiasa  wazalendo nchini wameunga mkono msimamo wa Tanzania uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na chokochoko zinazoanzishwa na Rwanda na wamemtaka Rais wa nchi hiyo, Paul Kagame, kukaa meza ya mazungumzo na waasi wa nchi hiyo walioko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwani amani haiwezi kutafutwa kwa njia ya mtutu wa bunduki.

CHADEMA kidedea:Makada wake wafutiwa shtaka la ugaidi.


KWA mara nyingine Mahakama Kuu, imetupilia mbali mashtaka ya ugaidi yaliyofunguliwa dhidi ya viongozi na wananchama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Jana, Mahakama Kuu Kanda ya Tabora iliwafutia shtaka la ugaidi wanachama watano wa CHADEMA ikisema kosa lao ni la jinai na halipaswi kuitwa la ugaidi.

Monday

EAST AFRICAN COMMUNITY INAKUFA

Mimi siku zote husema si nabii wala mbashiri, sina ujuzi wa kutembelea nyota, lakini kwa mambo yote ambayo ninayaona kwa sasa, hakika ni alama mbaya , hatari kwa nchi yangu, Tanzania.
Hakuna shaka, pia ni hakika kwamba ni hatari pia hata kwa uhai na ustawi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa jumla wake.

MAMA WA KANUMBA ADAIWA KUUZA MAGARI YOTE YA MAREHEMU STEVEN KANUMBA NA PESA KUNYWEA POMBE


Inavyosemekana imebaki Hice tu ambayo nayo kesha pewa dalali atafute Mnunuzi. Ofisi nayo inapumulia mashine. kuna mazito ndani ya familia hiyo.


" NILIKURUPUKA KUOLEWA NA ABDULATIF FUNDIKIRA (TIFF) JACK PATRICK..


MWANAMITINDO marufu Bongo, Jacqueline Patrick ‘Jack’ amesema alikurupuka kuolewa na aliyekuwa mume wake, Abdulatif Fundikira ‘Tiff’ kwa kuwa hakufanya tathmini ya kina kabla ya kufanya maamuzi.
                                       Jack na mumewe
 

Forbes Africa imetoa Forbes Africa magazine model list Flaviana Matata ndani: Noma Sanaaa



Ikiwa imetangazwa siku chache zilizopita, Forbes Africa imetoa list ya ma-model wakali na wanaofanya vizuri, na model matata kutoka Tanzania "Flaviana Matata" ndani.

Ripoti ya mauji Arusha yavuja •IGP Mwema, RPC Andengenye watiwa hatiani.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

HATIMAYE ripoti ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kuhusu vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu na mauaji yaliyotokea Arusha Januari 5, 2011 kwenye maandamano ya CHADEMA imevuja.


Licha ya ripoti hiyo kufichwa kwa kutosomwa hadharani kwenye vyombo vya habari kutokana na kulishutumu moja kwa moja Jeshi la Polisi, Tanzania Daima imefanikiwa kuinasa.

SIKU YA JANA, ILIKUA MBAYA KWA ARSENAL WENGER BAADA YAKUFUNGWA


  Amefunga: Drogba amefunga mabao dakika za lala salama Kombe la Emirates
 
MSHAMBULIAJI Didier Drogba ameendelea kuwa mwiba kwa Arsenal akikumbushia enzi zake alipokuwa na jezi ya Chelsea, baada ya mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 35 siku ya jana kufunga mabao mawili na kuiwezesha klabu yake, Galatasaray kutwaa Kombe la Emirates.
 

FEZA APONA BIG BROTHER THE CHASE, ONEL OUT

clip_image002 
 
Homa iliyokuwa ikiwakabili watanzania kwamba huenda muwakilishi pekee kutoka Tanzania, Feza Kessy siku zake zimeisha kutoka kwenye jumba la Big Brother imepata tiba usiku huu ambapo muwakilishi huyo, amebaki bali mpenzi wake Oneal kutoka Botswana, ndio ametoka.

HUJUI KUTONGOZA???...... SOMA HAPA NAMNA YA KUTONGOZA MSICHANA YOYOTE



  Muda au Pesa Nyingi!"
   Kutongoza ni sanaa ya ushawishi, ambayo lengo lake ni kuanzisha mahusiano ya karibu. Kuna sanaa zingine za ushawishi kama vile ushawishi wa kibiashara ambapo lengo ni kuuza bidhaa. Na kuna ushawishi wa kisiasa ambapo lengo ni kupata kura.
   Wakati sanaa karibia zingine zote za ushawishi ni rahisi kujifunza, sanaa ya kutongoza watu wengi wanasema eti haifundishwi ... eti kila mwanaume anajua kutongoza.

USAJILI WA WACHEZAJI WA LIGI KUU MWISHO AGOSTI 5


Usajili wa wachezaji kwa hatua ya kwanza msimu huu (2013/2014) sasa utafungwa Jumatatu (Agosti 5 mwaka huu) badala ya Agosti 3 mwaka huu kama ilivyokuwa imepangwa awali.

WABUNGE WACHAPANA NGUMI ZA KAVU KAVU BUNGENI


Picha: Ni wabunge wa Taiwan 'walivyoadabishana' jana baada ya kupishana maelewano kufuatia mpango wa kupiga kura ya maoni iliyoazimia kuidhinisha umaliziwaji wa mradi wa nne wa Nyuklia katika kisiwa ambacho kinakaliwa na watu wapatao milioni 23.

RAIS KIKWETE AWAPA WANYARWANDA SIKU 14 ZA KUONDOKA TANZANIA. ***MAMIA WAANZA KUREJEA RWANDA


Mamia ya wahamiaji haramu kutoka nchini Rwanda wakiwa na ng’ombe zaidi 900 wameanza kuondoka nchini kurejea kwao kutokana na agizo la Rais Jakaya Kikwete kuwataka waondoke Tanzania kabla ya siku 14.