Recent Posts

coments

HOT HEAD LINES

NEWS+HABARI-ZAIDI

ALL HERE DONE BY |

ALL HERE DONE BY |

**ADVERTISEMENT**

**ADVERTISE**

**ADVERTISE**

HAPPY BIRTH DAY

HAPPY BIRTH DAY
Powered by Blogger.

LAANA: WATUMIA VAZI LA MASISTER WA KANISA KUSAFIRISHIA MADAWA YA KULEVYA, HATIMAYE WANASWA AIRPORT

No comments


 
Wanawake watatu wamekamatwa kwa madai ya kujaribu kusafirisha dawa za kulevya kupitia uwanja wa ndege wakiwa wamevalia kama masista.
Wasafirishaji hao walisimamishwa wakati wakiwasili kwenye kituo maarufu cha mapumziko nchini Colombia, sababu polisi walifikiri kwamba mavazi yao hayakuwa yakionekana halisia.
Maofisa waligundua kwamba kila mwanamke kati yao alikuwa na zaidi ya kilo 4 za cocaine zikiwa zimefungwa katika miguu yake.
 
Wakiwaongezea fedheha katika mashitaka, wasafirishaji hao walipangwa mstari mbele ya waandishi wakiwa bado wamevalia mavazi yao ya kituko kuficha ukweli.
Wanawake hao watatu, wenye umri wa miaka 20, 32 na 37, walitua kwa ndege kwenye kisiwa hicho cha San Andres kutoka Bogota siku ya Jumamosi asubuhi.
Kapteni wa Polisi Oscar Davila alisema wanawake hao walionekana kama wamechanganyikiwa, na kuongeza kwamba mfumo wa tabia zao haukuonekana kuwa sahihi.

Pale masista hao bandia waliposimamishwa na kupekuliwa, walikutwa wakiwa na shehena kubwa ya cocaine ikiwa imefungwa katika miili yao.
Wote watatu waliangua kilio na kusisitiza kwamba walitumiwa tu kusafirisha dawa hizo sababu ya matatizo yao ya kifedha, alisema Davila.
Wanawake hao walikamatwa na kuswekwa rumande kwa mashitaka ya kusafirisha dawa za kulevya.
Dawa hizo zilikadiriwa kuwa na thamani ya Dola za Marekani 35,000 mtaani, kwa mujibu wa Kamishna wa Polisi wa mji huo, Jorge Gomez.
"Hawakuwa wafuasi halisi wa dini, hawakuwa masista," alisema. "Kinyume cha hilo, walikuwa wakitumia mwanya huo kwa ajili ya kazi hii.
"
San Andres, iliyoko Caribbean nje ya ufukwe wa Nicaragua, ni moja ya mahali maarufu kabisa nchini Colombia kwa ajili ya wakazi na watalii.
Hatahivyo, inatumika pia kama njia kuu ya kupitishia dawa za kulevya kwa ajili ya kusafirisha cocaine kati ya Colombia bara na Amerika ya Kati.
BONGO NEWS 4 NEWS#

No comments :

Post a Comment

Total Pageviews

About Us

Spice Mag - Premium free blogger template developed by spicytricks.com.

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas hendrerit iaculis nunc. Curabitur in eros ipsum. Pellentesque habitant morbi tristique senectus et netus et malesuada fames ac turpis egestas. Duis at mi justo, non suscipit elit. Nunc aliquam luctus adipiscing. Nullam sit amet lacus vitae odio congue mollis eu non magna. Duis sed arcu a libero adipiscing rhoncus. Aliquam erat volutpat. Suspendisse sed nunc metus, sed aliquet arcu.

Ads 468x60px

Blog Archive

Followers

IN ENTERTAINMENT

ADVERTISE MENT

**ADVERTISE MENT**

**ADVERTISE MENT**

VIDEO OFTHE DAY (Diamond Platnumz - Number One (Official Video Music) )

TOP HEAD LINES