Mke anayedaiwa kupanga kumuua mumewe kortini
Arusha.
Mwanamke anayedaiwa kupanga njama za kumuua mumewe wa
ndoa na mtoto wa mume huyo, amepandishwa mahakamani akiwa na mtuhumiwa
mwingine wa mauaji hayo.
Janeth Jackson (32), mkazi wa Moshono, Arusha na Novatus Elias, walifikishwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha /Arumeru, Devotha Kamuzora, wakisomewa makosa mawili ya kula njama ya kutaka kumuua Simon Jackson ambaye ndiye mume wa Janeth.
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Edna Kasala, alidai mahakamani hapo kuwa washtakiwa wote walitenda kosa la pili la kula njama na kutaka kumuua Desderi Sabas, ambaye ni mtoto wa mke mwingine kwa mume huyo anayeishi Bukoba, mkoani Kagera.
Washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu lolote kwa sababu Mahakama hiyo kisheria haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.
Kasala iliomba mahakama kuwanyima dhamana washtakiwa, kwa sababu watuhumiwa wengine wawili wanatafutwa hivyo na upelelezi haujakamilika.
Alidai kutokana na uzito wa tuhuma hizo, maombi
hayo ya kuwanyima dhamana washtakiwa yameambatana na hati ya kiapo ya
Mkuu wa Upelelezi Makosa ya Jinai Mkoa wa Arusha.
“Mheshimiwa tunafahamu kwamba dhamana ni haki ya washtakiwa kikatiba, lakini kutokana na mazingira ya kesi hii kuwa magumu, tunaomba dhamana isitolewe ili kuwatafuta watuhumiwa wengine wa kesi hii,” alidai Kasala.
Kwa upande wake,Wakili wa utetezi, Fidelis Peter, alipinga maombi hayo na kutaka mahakama itoe dhamana kwa washtakiwa kwa sababu ni haki yao ya kikatiba na kwamba hilo ni kosa lao la kwanza.
Sababu nyingine ya kupinga maombi ya upande wa mashtaka, ni kwamba washtakiwa wanaweza kuvuruga upepelezi wakiachiwa siyo za msingi kwani ni watu wanaoaminika katika jamii.
“Mheshimiwa sababu za kuwanyima dhamana washtakiwa hazina uzito wowote, pia mshtakiwa wa kwanza (Janeth) ana mtoto wa miezi sita na tangu akamatwe alhamisi iliyopita hajamwona wala kumnyonyesha hivyo anastahili kupewa dhamana,”alidai Wakili Peter.
Hata hivyo, baada ya kusikiliza maombi ya pande zote mbili, Hakimu Kamuzora, alikubaliana na maombi ya upande wa mashtaka na kuamuru watuhumiwa wapelekwe mahabusu hadi Agosti 5, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
Katika kesi hiyo iliyovuta hisia za watu wengi jijini hapa, inadaiwa Janeth alitaka kumuua mumewe ambaye ni mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite na mwanaye wa kiume, ili arithi mali na utajiri alionao mfanyabiashara huyo.
Akiwa amejifunika uso muda wote alipokuwa mahakamani, Janeth
alionekana kuwa na mawazo mengi na macho mekundu kwa sababu ya kulia
baada ya njama hizo kugonga mwamba.
Awali kabla ya kukamatwa kwa mwanamke huyo, taarifa zilieleza kuwa, mwanamke huyo alitumia fedha nyingi kulipa majambazi waliotakiwa kutekeleza tukio hilo lakini mmoja wa majambazi hao aliamua kuvujisha siri hiyo polisi iliyofanikisha kukamatwa kwa wahusika kabla ya kutenda mauaji hayo.
Mume wa mwanamke huyo alinukuliwa awali akisikitika na kuhoji kwa nini mke huyo alifikia kupanga hilo.
CREDIT: MWANANCHI GAZETI
- Blogger Comments
- Facebook Comments
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
Total Pageviews
328707
About Us
Spice Mag - Premium free blogger template developed by spicytricks.com.
Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas hendrerit iaculis nunc. Curabitur in eros ipsum. Pellentesque habitant morbi tristique senectus et netus et malesuada fames ac turpis egestas. Duis at mi justo, non suscipit elit. Nunc aliquam luctus adipiscing. Nullam sit amet lacus vitae odio congue mollis eu non magna. Duis sed arcu a libero adipiscing rhoncus. Aliquam erat volutpat. Suspendisse sed nunc metus, sed aliquet arcu.
Recent Posts
Ads 468x60px
Blog Archive
Followers
IN ENTERTAINMENT
SERENGETI FIESTA 2013 MKOANI MTWARA NOOOOOMAAAA SAAAANAAAAA
Wakazi wa Mtwara wajitokeza kwa wingi katika Tamasha la Burudani la...SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA, DIAMOND APOKONYWA PASSPORT.., MASANJA MKANDAMIZAJI NAYE YUPO
Ni mwendelezo wa Sakata la unga ambalo sasa ni janga kwa taifa letu. Orodha...VIDEO YA YALIO JIRI UZINDUZI WA VIDEO MPYA YA DIAMOND "NUMBER ONE"
DIAMOND AKI ONGEA NA WAANDISHI WA HABARI Penny Mungilwa - Number 1...
ADVERTISE MENT
**ADVERTISE MENT**

Pages
VIDEO OFTHE DAY (Diamond Platnumz - Number One (Official Video Music) )
STAR VOTE
TOP HEAD LINES
-
Muda au Pesa Nyingi!" Kutongoza ni sanaa ya ushawishi, ambayo lengo lake ni kuanzisha mahusiano ya karibu...
-
PRODYUZA mkali Bongo, Manaiki Sanga amekumbwa na skendo ya aibu kufuatia picha zake ...
-
MUZIKI ni kazi, mataifa mengi, hususan katika mabara ya Ulaya na Amerika Kaskazini, ume...
-
Usajili wa wachezaji kwa hatua ya kwanza msimu huu (2013/2014) sasa utafungwa Jumatatu (Agosti 5 mwaka huu) badala ya Agosti 3 mwa...
No comments :
Post a Comment