Recent Posts

coments

HOT HEAD LINES

NEWS+HABARI-ZAIDI

Archive

ALL HERE DONE BY |

ALL HERE DONE BY |

**ADVERTISEMENT**

**ADVERTISE**

**ADVERTISE**

HAPPY BIRTH DAY

HAPPY BIRTH DAY
Powered by Blogger.

MBWANA SAMATA ANATISHA AZIDI KULITANGAZA JINA LA TANZANIA KWENYE SOKA.

No comments

Samatta

Yawezekana Taifa Stars ikawa haifanyi vizuri kwenye michuano ya kimataifa kiasi cha kuwa chini kwenye chati za soka barani Afrika na duniani kwa ujumla lakini jina la Taifa hili limekuwa likitajwa na lina uhakika wa kutajwa katika level za juu za soka barani afrika, hii ni kutokana na makubwa yanayofanywa na kijana mwenye umri wa miaka 21 raia wa Tanzania ambaye ni Mbwana Samatta .
Mchezaji huyu ambaye anacheza nafasi ya ushambuliaji amekuwa akifanya vizuri sana kwenye klabu yake ya Tp Mazembe ya Nchini Congo DRC kwenye michuano ya kimataifa na amekuwa na mchango mkubwa sana kwenye michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika .
Samatta alifunga bao moja kwenye mechi iliyochezwa jana kati ya timu yake ya Tp Mazembe na FUS Rabat ambapo Mazembe ilishinda 3-0 na mpaka sasa Samatta amekuwa akifunga kwenye mechi zote nne za michuano hiyo ambazo Mazembe imecheza hali inayomfanya awe na nafasi kubwa ya kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo wakati ikimalizika baadaye mwaka huu.
Mbwana Samatta akiwa anasaini Autograph za mashabiki wa soka Ivory Coast ambao walivutiwa na uwezo wake wakati wa mazoezi ya Taifa Stars nchini humo.
Mbwana Samatta akiwa anasaini Autograph za mashabiki wa soka Ivory Coast ambao walivutiwa na uwezo wake wakati wa mazoezi ya Taifa Stars nchini humo.
Samatta ambaye Mazembe ilimsajili toka Simba Sports Club ya Tanzania ameendelea kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania na amekuwa na rekodi nzuri sana ya kufunga karibu kila mechi ambayo anacheza kwenye klabu hiyo .
Samatta amefanya watanzania wengi kuwa na shauku ya kufahamu matokeo ya timu ya Tp Mazembe ambapo mara zote watu huuliza timu hiyo imeshinda au la na baada ya kuuliza hivyo huuliza tena Samatta amefunga mangapi kwa kuwa wana uhakika juu ya uwezo wake na rekodi yake ya kuzifumania nyavu.
Ubora wake umemfanya kuishi maisha ya kistaa akiwa nchini Kongo ambapo mashabiki wa Mazembe wanampenda kiasi cha kutaka kupiga naye picha kila wamwonapo mtaani na wakati mwingine kutakakusukuma gari lake wanapoliona.
BONGO NEWS 4 NEWS#

No comments :

Post a Comment

Total Pageviews

About Us

Spice Mag - Premium free blogger template developed by spicytricks.com.

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas hendrerit iaculis nunc. Curabitur in eros ipsum. Pellentesque habitant morbi tristique senectus et netus et malesuada fames ac turpis egestas. Duis at mi justo, non suscipit elit. Nunc aliquam luctus adipiscing. Nullam sit amet lacus vitae odio congue mollis eu non magna. Duis sed arcu a libero adipiscing rhoncus. Aliquam erat volutpat. Suspendisse sed nunc metus, sed aliquet arcu.

Ads 468x60px

Blog Archive

Followers

IN ENTERTAINMENT

ADVERTISE MENT

**ADVERTISE MENT**

**ADVERTISE MENT**

VIDEO OFTHE DAY (Diamond Platnumz - Number One (Official Video Music) )

TOP HEAD LINES