Recent Posts

coments

HOT HEAD LINES

NEWS+HABARI-ZAIDI

Archive

ALL HERE DONE BY |

ALL HERE DONE BY |

**ADVERTISEMENT**

**ADVERTISE**

**ADVERTISE**

HAPPY BIRTH DAY

HAPPY BIRTH DAY
Powered by Blogger.

LHRC: Tutamshtaki Waziri Mkuu mahakamanig

No comments

Waziri Mkuu,Mizengo Pinda 


“Pinda alitoa kauli ile kama msimamo wa Serikali, tulitarajia angefuta kauli yake aliyotoa bungeni ya kuwabariki polisi kupiga raia katika mkutano ulioisha wa Bunge la Bajeti lakini hakufanya hivyo,” alisema.

kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”

 
Alijibu: “Ni lilelile nililosema... Mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... Hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria. “Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... Wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... Maana tumechoka.”
Mkurugenzi wa Maboresho na Utetezi wa LHRC, Harold Sungusia alisema jana wakati akitoa ripoti ya utafiti ya miezi sita kuhusu mambo mbalimbali ya haki za binadamu kuwa kituo hicho kiko katika hatua za mwisho za kupeleka shauri hilo Mahakama Kuu ili kumfungulia kesi Waziri Mkuu.
“Kauli ya Pinda inavunja Katiba ya nchi ya usawa mbele ya sheria ambayo ni Ibara ya 13 (1). Hivyo tumekusudia kumfungulia kesi Waziri Mkuu ambaye amevunja Katiba,” alisema.
Sungusia alisema kauli hiyo iliyotolewa na kiongozi wa juu wa Serikali ni kinyume cha Katiba, sheria za nchi na misingi ya haki za binadamu hivyo.
“Pinda alitoa kauli ile kama msimamo wa Serikali, tulitarajia angefuta kauli yake aliyotoa bungeni ya kuwabariki polisi kupiga raia katika mkutano ulioisha wa Bunge la Bajeti lakini hakufanya hivyo,” alisema.
Ofisi ya Waziri Mkuu wajibu
Akizungumza madai hayo jana, Katibu wa Waziri Mkuu, Deusdedit Buberwa alisema: “Hayo unayoniambia ni mapya kabisa. Mimi sifahamu chochote, kwani sijaona hata barua yao. Ningeweza kuzungumza kama ningepata barua au hata kusikia, lakini hakuna hicho kitu.”
Utafiti wa mauaji
Akitoa taarifa ya utafiti huo, Mtafiti wa LHRC, Pasience Mloe alisema katika kipindi cha miezi sita mwaka huu, kumekuwa na vifo 303 vilivyotokana na imani za kishirikina.
Alisema idadi hiyo ni kubwa kwani inakaribia sawa na takwimu za mwaka mzima wa 2012 ambao watu 336 walipoteza maisha kwa sababu hizohizo.
Mloe alisema utafiti huo ulibaini kuongeza kwa ubakaji wa watoto kwani katika kipindi hicho cha miezi sita, 394 walifanyiwa ukatili huo.
Alisema utafiti huo uligundua kuwa watoto hawana ulinzi wa kutosha hali ambayo inachangia vitendo hivyo kuongezeka kwa kasi kubwa.
“Tunataka Serikali ije na mikakati ambayo itasaidia kuondoa tatizo hili ambalo limekuwa kubwa na watu wengi wameuliwa,” alisema Mlowe
BONGO NEWS 4 NEWS#

No comments :

Post a Comment

Total Pageviews

About Us

Spice Mag - Premium free blogger template developed by spicytricks.com.

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas hendrerit iaculis nunc. Curabitur in eros ipsum. Pellentesque habitant morbi tristique senectus et netus et malesuada fames ac turpis egestas. Duis at mi justo, non suscipit elit. Nunc aliquam luctus adipiscing. Nullam sit amet lacus vitae odio congue mollis eu non magna. Duis sed arcu a libero adipiscing rhoncus. Aliquam erat volutpat. Suspendisse sed nunc metus, sed aliquet arcu.

Ads 468x60px

Blog Archive

Followers

IN ENTERTAINMENT

ADVERTISE MENT

**ADVERTISE MENT**

**ADVERTISE MENT**

VIDEO OFTHE DAY (Diamond Platnumz - Number One (Official Video Music) )

TOP HEAD LINES