WILAYA ya Arumeru mkoani Arusha kujenga uwanja wa kisasa wa soka.
WILAYA ya Arumeru mkoani Arusha iko mbioni kujenga uwanja mkubwa
wa kisasa wa soka ikiwa ni mpango mkakati wa kuendeleza michezo
wilayani hapa baada ya kufanikiwa kuwa na timu nyingi za vijana.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya hiyo (DC), Nyerembe Munasa,
wakati akizungumza katika hafla ya utoaji zawadi kwa mabingwa wa ligi
maalumu ya vijana Arumeru, iliyoanzishwa na mdau wa michezo kutoka
nchini Ufaransa, Damian Sellier, katika mji mdogo wa Usa River, eneo la
Liganga.
DC Nyerembe alisema, hiyo ni mikakati yake katika kukuza michezo kwa
kushirikiana na Halmashauri ya Meru, ambako tayari eneo la ujenzi
limepatikana na kinachofuata ni mipango ya ukusanyaji fedha kwa ajili ya
ujenzi huo kuanza.
Alifafanua kuwa katika mpango huo, kabla ya ujenzi kukamilika, hivi
sasa wataanzisha mashindano ya vijana wadogo kutafuta vijana 20 bora,
ambao watakuwa waanzilishi wa timu maalumu ya wilaya, ambayo mwakani
itapelekwa nchini Brazil kwa ajili ya mafunzo maalumu.
“Tayari nimeishapata baadhi ya wadhamini kusaidia mpango wa kukuza
soka kwa vijana na tumekubaliana kuanzia na vijana 20, ambao watapelekwa
nchini Brazil kwa ajili ya mafunzo maalumu, ili wakirudi wawe ndio
mfano kwa soka la nchi hii,” alisema Munasa.
Aidha, kupitia Halmashauri ya Meru, waliahidi mara baada ya kumalizika
kwa mashindano hayo juzi, wataanza kuukarabati uwanja wa Ngarasero, kwa
kuukwangua na kuweka udongo mpya kisha kupanda majani ili uwe na hadhi
stahiki kutumika katika mechi mbalimbali.
Naye Mratibu wa kituo cha Usa River Youth, ambao ndio walikuwa
wasimamizi wa ligi hiyo, Daudi Mkumba, licha ya kumshukuru DC Nyerembe
na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru kwa ushirikiano wao, aliwaomba
kuhakikisha wanatoa ushirikiano zaidi kwa taasisi zinazoanzisha
mashindano ya vijana ili kukuza na kuibua vipaji.
Katika mashindano hayo, timu ya Charky U-20 na ile ya U-15 waliibuka
mabingwa na kuambulia kombe na mipira, kabla ya DC Nyerembe kutoa sh
200,000.
- Blogger Comments
- Facebook Comments
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
Total Pageviews
328700
About Us
Spice Mag - Premium free blogger template developed by spicytricks.com.
Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas hendrerit iaculis nunc. Curabitur in eros ipsum. Pellentesque habitant morbi tristique senectus et netus et malesuada fames ac turpis egestas. Duis at mi justo, non suscipit elit. Nunc aliquam luctus adipiscing. Nullam sit amet lacus vitae odio congue mollis eu non magna. Duis sed arcu a libero adipiscing rhoncus. Aliquam erat volutpat. Suspendisse sed nunc metus, sed aliquet arcu.
Recent Posts
Ads 468x60px
Blog Archive
Followers
IN ENTERTAINMENT
SERENGETI FIESTA 2013 MKOANI MTWARA NOOOOOMAAAA SAAAANAAAAA
Wakazi wa Mtwara wajitokeza kwa wingi katika Tamasha la Burudani la...SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA, DIAMOND APOKONYWA PASSPORT.., MASANJA MKANDAMIZAJI NAYE YUPO
Ni mwendelezo wa Sakata la unga ambalo sasa ni janga kwa taifa letu. Orodha...VIDEO YA YALIO JIRI UZINDUZI WA VIDEO MPYA YA DIAMOND "NUMBER ONE"
DIAMOND AKI ONGEA NA WAANDISHI WA HABARI Penny Mungilwa - Number 1...
ADVERTISE MENT
**ADVERTISE MENT**

Pages
VIDEO OFTHE DAY (Diamond Platnumz - Number One (Official Video Music) )
STAR VOTE
TOP HEAD LINES
-
Muda au Pesa Nyingi!" Kutongoza ni sanaa ya ushawishi, ambayo lengo lake ni kuanzisha mahusiano ya karibu...
-
PRODYUZA mkali Bongo, Manaiki Sanga amekumbwa na skendo ya aibu kufuatia picha zake ...
-
MUZIKI ni kazi, mataifa mengi, hususan katika mabara ya Ulaya na Amerika Kaskazini, ume...
-
Usajili wa wachezaji kwa hatua ya kwanza msimu huu (2013/2014) sasa utafungwa Jumatatu (Agosti 5 mwaka huu) badala ya Agosti 3 mwa...
-
Kujichua au kujichezea(kupiga puri au punyeto) sio kwa wanaume tu bali hata wanawake wanafanya hivyo ila wengi wao huwa hawako hur...
No comments :
Post a Comment